JESHI LA POLISI LATOA MAFUNZO SHULE ZA MSINGI JIJINI


Ofisa polisi wa Usalama Barabarani (CPL) Rashid Msuya akiwafundisha wanafunzi wa Shule ya Msingi Mapambano Sinza jijini Dar es Salaam jinsi ya kuvuka barabara kwa kutumia alama za barabarani, ikiwa ni mwendelezo wa  kuadhimisha siku ya Afya na Usalama kazini Duniani. Hafla hiyo iliandaliwa na Vodacom Tanzania na kufanyika katika shule hapo.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Msasani A na B ya jijini Dar es Salaam,wakimsikiliza Ofisa polisi wa Usalama Barabarani (CPL) Rashid Msuya alipofika shuleni hapo pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom…
Ofisa polisi wa Usalama Barabarani (CPL) Rashid Msuya akiwafundisha wanafunzi wa Shule ya Msingi Mapambano Sinza jijini Dar es Salaam jinsi ya kuvuka barabara kwa kutumia alama za barabarani, ikiwa ni mwendelezo wa  kuadhimisha siku ya Afya na Usalama kazini Duniani. Hafla hiyo iliandaliwa na Vodacom Tanzania na kufanyika katika shule hapo.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Msasani A na B ya jijini Dar es Salaam,wakimsikiliza Ofisa polisi wa Usalama Barabarani (CPL) Rashid Msuya alipofika shuleni hapo pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania(Hawapo pichani) kwa ajili ya kutoa mafunzo ya Usalama  barabarani.
Mkuu wa Kitengo cha Afya na Usalama wa Vodacom Tanzania Karen Lwakatare (kushoto) akiwafafanulia jambo baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Mapambano.
Koplo Theresia Bayona akitoa elimu ya sheria za barabarani kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Msasani A na B iliyopo jijini Dar es Salaam.
Mwanafunzi wa darasa la pili Juma Rashid wa Shule ya Msingi Msasani A na B iliyopo jijini Dar es Salaam,akionesha ujumbe.
Gane Maikara kushoto na Patricia Stephano ambao ni Wanafunzi wa Shule ya Msingi Msasani A na B ya jijini Dar es Salaam,Wakifundishwa jinsi ya kuvuka barabara na Koplo Theresia Bayona (katikati).
Wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia wa shule ya msingi Msasani wakimsikiliza kwa makini mwalimu wao Selestina Msangi wakati akiwafafanulia jambo juu ya elimu ya utumiaji wa alama za barabarani.
Mustafa Hussein ambaye ni mwafunzi mwenye ulemavu wa kusikia katika shule ya msingi Msasani jijini Dar es Salaam (mwenye tisheti ya rangi ya damu ya mzee) akifafanuliwa jambo na Ofisa polisi wa Usalama Barabarani (CPL) Rashid Msuya,kuhusiana na sheria za alama za barabarani.
Ni katika mwendelezo wa kuadhimisha siku ya Afya na Usalama Duniani
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mapambano na Msasani A na B zote za jijini Dar es Salaam leo wamenufaika na mafunzo ya Afya na Usalama barabarani ikiwa ni mwendelezo wa kuadhimisha siku ya Afya na Usalama mahala pa kazi duniani na baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na jeshi la Polisi Kanda ya Mkoa wa Kinondoni jijini Dar es Salaam ambapo elimu hii pia itaendelea kutolewa katika shule za msingi zingine jijini mapema wiki hii.
Mafunzo hayo yaliyotolewa na wafanyakazi wa kampuni hiyo yalionekana kuwavutia wanafunzi wa shule hiyo ambao  pia walishiriki katika mazoezi ya kukabiliana na  majanga mbalimbali yanayojitokeza kwa dharura.
Akiongea juu ya mafunzo Mkuu wa Idara ya Afya na Usalama wa Vodacom Tanzania Karen Lwakatare,amesema Vodacom ikiwa ni kampuni inayozingatia usalama wa wafanyakazi wake na watanzania wote kwa ujumla imeamua kutoa mafunzo ya usalama sehemu za kazi kwa wanafunzi ikiamini kuwa wao ndio wafanyakazi wa baadaye ambao ndio tegemeo la kukua kwa uchumi wetu.
“Tumeona pia kuna umuhimu kwa wanafunzi hawa kujua alama mbali mbali za barabarani pamoja na matumizi yake mbali na kuishia kuziona tu kwa macho. Kama suala la usalama barabarani lazima lipewe kipaumbele kwani kama tujuavyo jiji la Dar es Salaam lina changamoto nyingi ukizingatia magari sasa yamekuwa mengi kitu na matumizi ya barabara yanachanganya watu wengi na kusababisha kuwepo na ajali nyingi za barabarani”.Alisema.

0 Comments