MTOTO WA MIAKA 13 AJIUNGA CHUO KIKUU- GHANA


Binti wa miaka 13, Ruth Ama Gyan-Darkwa amevunja rekodi kuwa mwanafunzi mdogo zaidi kuwahi kujiunga na Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Kwame Nkrumah nchini Ghana. Mwanafunzi huyu anasoma Shahada ya Kwanza ya Sayansi, akichukulia Hisabati kama somo kuu.

0 Comments